Skip to main content

KICHEFUCHEFU NA KUTAPIKA WAKATI WA UJAUZITO

Kichefuchefu na Kutapika sana wakati wa ujauzito
Dr. DALUS

Ni hali kali na inayoweza kutokea kwa mama mjamzito inayoambatana na kichefuchefu na kutapika sana au kwa namna nyingine ni kitendo endelevu cha kutapika wakati wa ujauzito kunakosababisha kupoteza uzito zaidi ya asilimia 5 ya uzito wa awali.
Huweza kupelekea kupoteza uzito, kuwa na lishe duni na kuharibika kwa usawia wa giligili, na kuharibika usawa wa kemikali mbalimbali mwilini.

Tatizo hili huambatana na kiwango kikubwa cha homoni ya HCG ambayo hutolewa kwenye kifuko cha mimba. Ukubwa wa tatizo Hutokea sana kwenye wiki 8 hadi 12 za ujauzito, na dalili hupotea wiki ya ishirini kwa wengi lakini asilimia 10 ya wenye tatizo hili.

Asilimia 0.3 hadi 2 ya wanawake wanaopata mimba katika mwaka huathiriwa na tatizo hili.
Vihatarishi Kuwa na ndugu mwenye tatizo hili kama dada, binti wa mama mwenye tatizo hili huwa kwenye hatari ya kupata tatizo hili.

Historia ya tatizo kwenye ujauzito uliopita Mimba mapacha Kuwa na hali ya kijeni inayoitwa triploidy na trisomy Kuwa na ujauzito unaoitwa molar au kuwa na historia kwenye ujauzito uliopita Wanawake  wenye historia hizi pia huweza kupata tatizo hili.
Homa ya miendo Kipanda uso .
Magonjwa ya kiakili Kisukari wakati wa ujauzito .
Kiwango cha juu cha homoni ya thyroid Upungufu wa vitamin B .
Dalili Kupoteza uzito zaidi ya asilimia 5 kwenye ujauzito .
Kukaukiwa maji mwilini,

kunakosababisha kuongezeka kwa kiwango cha ketoni na kupata choo kigumu Lishe duni.
Kubadilika kwa ladha ya chakula Kuongezeka mara dufu hisia ya ubongo dhidi ya miendo .

Kubadilika kwa homoni kwa haraka wakati wa ujauzito .
Vitu vilivyomo kwenye tumbo kurudi juu ya kinywa .
Msongo wa kimwili na hali Kuvia damu kwenye macho .
Kushindwa kufanya kazi za kila siku Kuweweseka/ndoto za mchana .

Matibabu .
Nia ya matibabu ni kutibu dalili na kuwa makini kwenye kiwango cha maji kwenye damu.
Kula chakula mara kwa mara kwa kiasi kidogo na kujizuia na vyakula vinavyosababisha kichefuchefu na kutapika huwa ni jambo la muhimu.

Chai ya tangawizi imekuwa ikitumiwa zamani na hutoa uahueni sana.
Matumizi ya vitamin B6 huwa ya msingi pia kwa utibu dalili hizi kuna matibabu mengine ya kusisimua mishipa ya fahamu kupitia ngozi yanayoweza kufanyika kwenye baadhi ya hospitali hapa duniani.

Dawa za kuzuia kichefuchefu na kutapika hushauriwa kutumiaka endapo hakuna njia nyingine baada ya kupata giligili-maji ya kutosha kupitia mishipa.
Dawa kama metroclopramide, phenothiazine na ondansetron ni dawa nzuri na huwa salama kipindi cha ujauzito.
Dawa za steroid za mishipa hutumika kwa wagonjwa ambao wameshindwa kusaidiwa na dawa za kuzuia kutapika.

Mwisho kuwekewa chakula kwa njia ya mishipa hutumika kwa wagonjwa ambaowanashindwa kuwa na uzito unaotakiwa kwa sababu ya kutapika sana japokuwa naapata matibabu.

Comments

Popular posts from this blog

BIMA YA AFYA NA FAIDA ZAKE

BIMA YA AFYA NA FAIDA ZAKE By Dalus Bima ya afya ni nini? Bima ya afya ni mfumo wa kujiunga kwa hiari ama kwa lazima unaomhakikishia mwanachama kugharamiwa gharama zozote zinazojitokeza katika kupata huduma za kiafya zikiwemo kumwona daktari, kufanya vipimo pamoja na kupata matibabu na dawa kwa mwanachama husika. Bima ya afya ni kama mkataba unaoingiwa na anayetaka huduma pamoja na mtoa huduma kwa kupitia mifuko au taasisi inayowaunganisha mtoa huduma pamoja na mhitaji wa huduma husika. Mara nyingi Bima ya afya hujumuishwa kwenye makato anayoyatoa mwajiri kwa waajiriwa wake katika kufanya malipo. Pia zipo bima zinazowahusu watu binafsi, wazee na wasiojiweza, wajawazito na wengine wenye mahitaji maalumu bila kusahau wanafunzi kipindi cha masomo yao. Mara nyingi wanachama huchagua taasisi ama mifuko inayotoa bima hizi kulingana na aina, viwango na mipaka (coverage) ya Taasisi/Bima hizo. Ni ukweli uliowazi kuwa kila mfuko huweza kutofautiana na mingine katika huduma inazozitoa kwa...

FAIDA ZA NDIZI MWILINI

FAIDA ZA NDIZI MWILINI Ndizi mbivu ni tunda linalotumika sana kama mlo sehemu mbalimbali duniani. Ni tunda ambalo ni tamu na lenye virutubisho mbalimbali na muhimu kwa mwili. Baadhi ya faida za ndizi kiafya ni kusaidia moyo kufanya kazi vizuri, kupunguza uwezekano wa kupata saratani na pumu. Ndizi ni chanzo kizuri cha madini ya Potasiamu. VIRUTUBISHO VILIVYOMO KWENYE NDIZI Ndizi ya wastani ina uzito wa kama gramu 126O. Ina nishati kiasi cha kalori 110, gramu 30 za wanga na gramu 1 ya protini. Ndizi hazina fati, lehemu (cholesterol) au madini ya Sodiamu. Ndizi zina virutubisho  vifuatavyo; Vitamini B6 – 0.5 mg Manganizi- 0.3 mg Vitamini C – 9 mg Potasiamu – 450 mg Kambakamba- 3g Protini – 1 g Magneziamu – 34 mg Madini ya Foliki- 25.0 mcg Riboflavin – 0.1 mg Niacin – 0.8 mg Vitamini A – 81 IU Madini ya chuma – 0.3 mg FAIDA ZA NDIZI KIAFYA Kushusha Shinikizo la Damu Ndizi zina madini ya Potasiamu kwa wingi amb...

MTOTO KATIKA UKUAJI

HATUA MUHIMU ZA UKUAJI WA MTOTO KISAIKOLOJIA Dr. DALUS Mtoto anapitia mabadiliko mbali mbali ya kimwili,kiakili na kisaikolojia pindi anapokua anakuwa hadi kuwa mtu mzima. leo nitakuelezea hatua za ukuaji wa mtoto kisaikolojia muhimu sana katika malezi yake. hatua hizo ni kama ifatavyo 1.ORAL STAGE Mtoto anakua katika stage hii anapokuwa na umri wa,mwezi mmoja hadi mwaka mmoja.   Sasa kwa kipindi hiki erogenous zone ya mtoto inakua mdomoni, raha ya mtoto inakua kitu chochote kinachoingia mdomoni ndo maaana kipindi hiki mtoto kila kitu anachoshika anapeleka mdomoni . Hiki ndo kipindi cha kujenga strong bond kwa mtoto na mama pale mtoto anapokuwa ananyonya inamjenga kumthamini mama kuliko mtu yyte Kipindi hiki inabdi kuwa makini na vitu kama shanga,sarafu nk ambavyo akiweka mdomoni vnaweza kumkaba Hapa kama mzazi ana tabia ya kula kucha ndo kipindi mtoto nae anajifunza na kua hvo anapokua 2.ANAL STAGE Stage hii inaanza umri wa mwaka 1 hadi miaka mi 3 Hapa mtoto raha yake ni ...