Skip to main content

FAIDA ZA TENDE

Zijue faida za kula tende kiafya
Tende ni matunda maarufu sana kutokana na faida kedekede zipatikanazo. Kwa kingereza huitwa dates, kwa kihindi huitwa khajur, kwa lugha ya kitaalamu (botanical name)huitwa Phoenix dactiylifera.
Tende zimetunukiwa viambata muhimu mno kama protini, wanga, vitamins B1, B3,B5,A1,pia madini kama kalsiam, magniziam, manganizi, na kopa.
Tende zinaweza kuchanganywa na maziwa ili kuongeza ufanisi, au kuchanganya na asali, unaweza kufanya juisi ya tende maridhawa, au kula hivi hivi. Miongoni mwa faida zinazopatikana kwa kutumia juisi ya tende au tende zenyewe ni kama ifuatavyo;
Kuimarisha mifupa (bones),misuli na meno, tende husaidia sana kuimarisha afya ya mifupa, misuli na meno ya mlaji. Sababu tende zina manganese kwa wingi, kalsiam, selenium, pamoja na copper.
Husaidia kuimarisha afya ya macho (eye sight), ulaji wa tende au juisi yake maridhawa. Kutokana na upatikanaji wa vitamini kwa wingi. Husaidia kwa wenye saratani. Kama ambavyo tafiti iliyofanywa na American cancer society, ambayo inaonesha mchango wa tende katika kupambana na saratani.
Husaidia kuongeza nguvu (nishati) au energy booster).kula tende japo tatu au juisi ya tende ili kuongeza nishati katika mwili wako. Tende zina sukari ya asili kama glucose, fructose na sucrose Hivyo humfanya mlaji kupata nishati ya kutosha na kwa haraka.
Husadia mfumo wa mmeng'enyo (digestive system). Kama unapata choo kigumu au matatizo yanayofungamana na mfumo wa mmeng'enyo  jenga tabia ya kula tende japo tatu kwa siku.
Tende zina dietary fibers (nyuzinyuzi )hivyo kuboresha usagaji wa chakula. Hupunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo. Tende zinasaidia kwa mlaji wake kuweza kuepukana na magonjwa ya moyo, pendelea kutumia juisi ya tende. Kuboresha afya ya ngozi yako, kuifanya iwe kwenye ubora wake.
Tende zimetunukiwa vitamin B5,ambavyo huzifanya seli za ngozi zilizokufa kuwa hai.
Husaidia kuimarisha afya za wanandoa hasa wanaume, na kupunguza tatizo la udhaifu katika jimai (sexual under performance). Tende zinakiwango kikubwa cha estradiol na flavonoids ambavyo huongeza uzalishaji wa mbegu (sperms)  changanya tende, maziwa na asali.
Pia husaidia kuondoa tatizo la ugumba (sterility).

Comments

Popular posts from this blog

BIMA YA AFYA NA FAIDA ZAKE

BIMA YA AFYA NA FAIDA ZAKE By Dalus Bima ya afya ni nini? Bima ya afya ni mfumo wa kujiunga kwa hiari ama kwa lazima unaomhakikishia mwanachama kugharamiwa gharama zozote zinazojitokeza katika kupata huduma za kiafya zikiwemo kumwona daktari, kufanya vipimo pamoja na kupata matibabu na dawa kwa mwanachama husika. Bima ya afya ni kama mkataba unaoingiwa na anayetaka huduma pamoja na mtoa huduma kwa kupitia mifuko au taasisi inayowaunganisha mtoa huduma pamoja na mhitaji wa huduma husika. Mara nyingi Bima ya afya hujumuishwa kwenye makato anayoyatoa mwajiri kwa waajiriwa wake katika kufanya malipo. Pia zipo bima zinazowahusu watu binafsi, wazee na wasiojiweza, wajawazito na wengine wenye mahitaji maalumu bila kusahau wanafunzi kipindi cha masomo yao. Mara nyingi wanachama huchagua taasisi ama mifuko inayotoa bima hizi kulingana na aina, viwango na mipaka (coverage) ya Taasisi/Bima hizo. Ni ukweli uliowazi kuwa kila mfuko huweza kutofautiana na mingine katika huduma inazozitoa kwa...

FAIDA ZA NDIZI MWILINI

FAIDA ZA NDIZI MWILINI Ndizi mbivu ni tunda linalotumika sana kama mlo sehemu mbalimbali duniani. Ni tunda ambalo ni tamu na lenye virutubisho mbalimbali na muhimu kwa mwili. Baadhi ya faida za ndizi kiafya ni kusaidia moyo kufanya kazi vizuri, kupunguza uwezekano wa kupata saratani na pumu. Ndizi ni chanzo kizuri cha madini ya Potasiamu. VIRUTUBISHO VILIVYOMO KWENYE NDIZI Ndizi ya wastani ina uzito wa kama gramu 126O. Ina nishati kiasi cha kalori 110, gramu 30 za wanga na gramu 1 ya protini. Ndizi hazina fati, lehemu (cholesterol) au madini ya Sodiamu. Ndizi zina virutubisho  vifuatavyo; Vitamini B6 – 0.5 mg Manganizi- 0.3 mg Vitamini C – 9 mg Potasiamu – 450 mg Kambakamba- 3g Protini – 1 g Magneziamu – 34 mg Madini ya Foliki- 25.0 mcg Riboflavin – 0.1 mg Niacin – 0.8 mg Vitamini A – 81 IU Madini ya chuma – 0.3 mg FAIDA ZA NDIZI KIAFYA Kushusha Shinikizo la Damu Ndizi zina madini ya Potasiamu kwa wingi amb...

MTOTO KATIKA UKUAJI

HATUA MUHIMU ZA UKUAJI WA MTOTO KISAIKOLOJIA Dr. DALUS Mtoto anapitia mabadiliko mbali mbali ya kimwili,kiakili na kisaikolojia pindi anapokua anakuwa hadi kuwa mtu mzima. leo nitakuelezea hatua za ukuaji wa mtoto kisaikolojia muhimu sana katika malezi yake. hatua hizo ni kama ifatavyo 1.ORAL STAGE Mtoto anakua katika stage hii anapokuwa na umri wa,mwezi mmoja hadi mwaka mmoja.   Sasa kwa kipindi hiki erogenous zone ya mtoto inakua mdomoni, raha ya mtoto inakua kitu chochote kinachoingia mdomoni ndo maaana kipindi hiki mtoto kila kitu anachoshika anapeleka mdomoni . Hiki ndo kipindi cha kujenga strong bond kwa mtoto na mama pale mtoto anapokuwa ananyonya inamjenga kumthamini mama kuliko mtu yyte Kipindi hiki inabdi kuwa makini na vitu kama shanga,sarafu nk ambavyo akiweka mdomoni vnaweza kumkaba Hapa kama mzazi ana tabia ya kula kucha ndo kipindi mtoto nae anajifunza na kua hvo anapokua 2.ANAL STAGE Stage hii inaanza umri wa mwaka 1 hadi miaka mi 3 Hapa mtoto raha yake ni ...