Skip to main content

Posts

Showing posts from April, 2018

FISTULA

FAHAMU ZAIDI KUHUSU FISTULA By Dr. DALUS Kwa kitaalamu fistula hujulikana kama njia isiyo ya kawaida inayounganisha mfuko wa mkojo na uke, ambayo huruhusu mkojo na/au haja kubwa kutoka  bila kujizuia kwenye kuta za uke. Nini hutokea? Tatizo la kushindwa kujizuia kujikojolea na/au kupitisha haja kubwa kwenye tupu ya mwanamke linalojulikana kama fistula hutokea baada ya mwanamke kupata madhara kipindi cha kujifungua kutokana na kuwa kwenye uchungu wa kujifungua kwa muda mrefu (Prolonged and obstructed labor), kutokana na kichwa cha mtoto kushindwa kupita kwa urahisi kwenye tupu ya  mwanamke. Hali hii husababisha tishu za kwenye tupu ya mwanamke, kibofu cha mkojo na puru (rectum), kugandamizwa kati ya kichwa cha mtoto na nyonga za mwanamke. Hii husababisha mfumo wa damu kwenye tishu hizi kuharibika na tishu kukosa damu na kuwa katika hali inayojulikana kitaalamu kama ischemic necrosis. Baadaye tundu hutokea kati ya tupu ya mwanamke na kibofu cha mkojo au kati ya tupu ya mwa...

DALILI ZA UJAUZITO

DALILI ZA UJAUZITO By Dr.  DALUS Dalili za ujauzito hutofautiana kati ya mwanamke mmoja  na mwanamke mwingine, ingawa kuchelewa au kukosa hedhi ni dalili moja muhimu sana ya ujauzito. Ni muhimu kuzitambua na kuzifahamu dalili hizi kwa sababu zinaweza kusaidia kujua kama kweli umeshika ujauzito au la  pamoja na kuweza kutofautisha matatizo mengine yanayoshahabiana kwa dalili na  ujauzito. Hebu sasa tuangalie dalili na ishara za ujauzito: Kutokwa damu kidogo ukeni wakati kiumbe kikipandikizwa kwenye mfuko wa uzazi, ingawa siyo wanawake wote hupatwa na dalili hii. Kukosa hedhi, hii ni moja ya dalili kubwa ya ujauzito . Maumivu kwenye matiti na kuvimba matiti (huweza kutokea kati ya wiki ya 1 hadi ya 2) Uchovu, wanawake wengi huhisi uchovu na  na hali ya kutopenda kufanya lolote. Kupoteza ladha au kuhisi ladha ya chuma mdomoni Kuongezeka kwa hisia ya harufu, kipindi cha ujauzito wanawake wengi huongezeka hisia ya harufu Kic...

BISHOP SCORE

Understanding Your Bishop Score and What to Expect from Labor Induction Medical. Written by Dr. DALUS The Bishop score Is a system used by medical professionals to decide how likely it is that you will go into labor soon. They use it to determine whether they should recommend induction, and how likely it is that an induction will result in a vaginal birth. The score considers different factors about your cervix and the position of your baby. Each factor is given a grade, and then these grades are added up to give you an overall score. It’s called the Bishop score because it was developed by Dr. Edward Bishop in the 1960s. SCORE Understanding your score There are several factors that your doctor will consider when calculating your score: Dilation of the cervix. This means how far your cervix has opened in centimeters. Effacement of the cervix. This means how thin your cervix is. It is normally about 3 centimeters long. It gradually becomes thinner as labor progresses. C...

KUHARIBIKA KWA MIMBA (Abortion)

KUHARIBIKA KWA MIMBA (Abortion) By Dr. DALUS Tatizo la mimba kutoka au kutolewa ni jambo ambalo limewakumba kina mama wengi walio katika umri wa kuzaa. Aidha mijadala kuhusu kuhalalishwa au kuendelea kuharamishwa kwa utoaji mimba ni jambo linalochukua nafasi ya mazungumzo ya kila siku katika maisha yetu. Kwa baadhi ya nchi, suala la utoaji mimba ni jambo lililohalalishwa kisheria ingawa kwa nchi kama Tanzania, suala hili halijahalalishwa isipokuwa tu pale panapokuwa na sababu za kitabibu zinazolazimisha kufanya hivyo. Nini maana ya mimba kutoka? Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), utokaji mimba (abortion) hutokea pale ambapo kiumbe (mimba) kilicho chini ya wiki 22 kinapotoka kwa sababu moja ama nyingine, au kinapotolewa kwa njia yeyote ile. Aidha shirika la Afya limekwenda mbali zaidi na kutoa maana nyingine ya utokaji mimba kuwa ni pale mtoto (kiumbe) anapozaliwa akiwa na uzito wa chini ya gram 500. Aidha baadhi ya matabibu hupendelea kutumia neno 'abortion' ...

MADHARA YA UNYWAJI YA POMBE WAKATI WA UJAUZITO

Madhara ya Unywaji wa Pombe wakati wa Ujauzito. By Dr. DALUS Kati ya mambo ambayo watu wengi hawatilii maanani sana ni unywaji wa pombe wakati wa ujauzito. Nimekuwa nikiwaona akina mama wajawazito wengi wakinywa pombe kwenye sehemu za starehe na sherehe mbalimbali. Hata hivyo si nia ya makala hii kuwazuia kunywa pombe bali kuwapa elimu sahihi juu ya unywaji wa pombe wakati wa ujauzito. Baadhi ya wataalam wanasema unywaji wa wastani wakati wa ujauzito ni kitu ambacho kinaweza kukubalika ingawa wapo baadhi ya wataalamu wengine wanaoamini kuwa unywaji wa hata glasi moja ya mvinyo (wine) kwa wiki huhatarisha afya ya mtoto wako. Hata hivyo haijulikani kwa hakika, ni kiasi gani cha pombe ni salama kwa makuzi sahihi ya mtoto wako tumboni. Wataalamu wengi wanashauri kuacha pombe kabisa wakati wa ujauzito. Pombe inaweza kuleta madhara makubwa kwa mtoto wako bila wewe kuhisi madhara yake. Na yanaweza kuwa madhara ya kudumu ambayo ataishi nayo maisha yake yote. Aidha kuna dhana imejengek...

KIFAFA CHA MIMBA (ECLAMPSIA)

TATIZO LA KIFAFA CHA MIMBA (ECLAMPSIA) By Dr. DALUS Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaohusiana na msukumo mkubwa wa damu (high blood pressure) wakati wa ujauzito pamoja na kuharibika kwa viungo muhimu mwilini kama vile figo na ini. Kwa kawaida ugonjwa huu hutokea baada ya nusu ya kwanza ya ujauzito kuisha (kuanzia wiki ya 20 au miezi mitano ya ujauzito). Ugonjwa huu huweza kuwatokea hata wajawazito ambao hawakuwa na tatizo la msukumo mkubwa wa damu kabla ya ujauzito. Ugonjwa wa kifafa cha mimba unaweza kuleta madhara makubwa kwa mjamzito na mtoto aliye tumboni. Kuharibika kwa viungo muhimu kama figo na ini la mjamzito kunaweza kuwa kwa kiwango kikubwa kichoweza kusababisha mjamzito kupoteza maisha iwapo hatapata huduma ya afya mapema. Vilevile mtoto aliye tumboni anaweza kuathirika kwa kukosa damu ya kutosha toka kwa mama na kushindwa kukua vizuri na iwapo hali hiyo ikiendelea muda mrefu anaweza kufia tumboni. Kutokana na hatari kubwa ya ugonjwa huu kwa wajawazito na watoto wali...

KICHEFUCHEFU NA KUTAPIKA WAKATI WA UJAUZITO

Kichefuchefu na Kutapika sana wakati wa ujauzito Dr. DALUS Ni hali kali na inayoweza kutokea kwa mama mjamzito inayoambatana na kichefuchefu na kutapika sana au kwa namna nyingine ni kitendo endelevu cha kutapika wakati wa ujauzito kunakosababisha kupoteza uzito zaidi ya asilimia 5 ya uzito wa awali. Huweza kupelekea kupoteza uzito, kuwa na lishe duni na kuharibika kwa usawia wa giligili, na kuharibika usawa wa kemikali mbalimbali mwilini. Tatizo hili huambatana na kiwango kikubwa cha homoni ya HCG ambayo hutolewa kwenye kifuko cha mimba. Ukubwa wa tatizo Hutokea sana kwenye wiki 8 hadi 12 za ujauzito, na dalili hupotea wiki ya ishirini kwa wengi lakini asilimia 10 ya wenye tatizo hili. Asilimia 0.3 hadi 2 ya wanawake wanaopata mimba katika mwaka huathiriwa na tatizo hili. Vihatarishi Kuwa na ndugu mwenye tatizo hili kama dada, binti wa mama mwenye tatizo hili huwa kwenye hatari ya kupata tatizo hili. Historia ya tatizo kwenye ujauzito uliopita Mimba mapacha Kuwa na hali ya kij...

PLACENTA ABRUPTION

TATIZO LA KONDO LA NYUMA (PLACENTA) KUACHIA KABLA YA MTOTO KUZALIWA (Placenta abruption) Miongoni mwa dharura zinazoweza kuwatokea baadhi ya wajawazito, ambayo husababisha mama kupoteza damu nyingi, kufa kwa mtoto na hata mama mwenyewe ni Placenta abruption. Neno Placenta abruptio humaanisha hali ya kujitenga kwa kondo la nyuma (placenta) kutoka sehemu ilipojishikilia kwenye ukuta wa tumbo la uzazi (uterus) kabla hata ya mtoto kuzaliwa. Kondo la nyuma au placenta ni kiungo kinachofanya kazi ya kumlisha mtoto akiwa tumboni kwa mama yake. Katika hali ya kawaida, kondo la nyuma hujitenga na ukuta wa mfuko wa uzazi mara baada ya mtoto kuzaliwa. Hali hii husababishwa na nini? Sababu hasa za hali hii zaweza kuwa ngumu kuzibaini ingawa baadhi ya visababishi hivyo vyaweza kuwa Kuumia eneo la tumbo kunakoweza kusababishwa na ajali za gari, kuangukia tumbo au kupata kipigo kikali Kupoteza kwa kiasi kikubwa cha maji yaliyo katika mfuko wa uzazi (amniotic fluid). Maji haya yanaweza kupotea ...

VYAKULA WAKATI WA UJAUZITO

FAHAMU VYAKULA VINAVYOFAA NA VILE VINAVYOZUILIWA WAKATI WA UJAUZITO Dr. DALUS Ni vyakula gani vya kuepuka kutumiwa na wajawazito? Ili mtoto azaliwe akiwa na afya njema pamoja na akili timamu, akiwa tumboni lazima alishwe lishe bora na mlo sahihi. Mwenye jukumu la kutoa lishe bora na sahihi kwa kiumbe kilichomo tumboni ni mama. Anatakiwa kujua aina ya vyakula anavyopaswa kula. Vivyo hivyo, anatakiwa kujua aina ya vyakula vya kuviepuka. Katika makala ya leo, tunaangalia orodha ya vyakula vilivyokatazwa. Mama mja mzito haruhusiwi kuvila vyakula vifuatavyo kwa faida ya kiumbe kilichomo tumboni na kwa faida yake mwenyewe: Nyama mbichi Epuka kula samaki au nyama mbichi au iliyopikwa lakini haikuiva vizuri. Utajiepusha na uwezekano wa kula bakteria na vijidudu vingine hatari kwa afya ya mtoto tumboni. Mjamzito anapokula nyama, anatakiwa kuhakikisha imeiva sawasawa. ‘Soseji” na “Sandwich” Mjamzito haruhusiwi kula ‘soseji’, ‘sandwichi’ za nya...

MTOTO KATIKA UKUAJI

HATUA MUHIMU ZA UKUAJI WA MTOTO KISAIKOLOJIA Dr. DALUS Mtoto anapitia mabadiliko mbali mbali ya kimwili,kiakili na kisaikolojia pindi anapokua anakuwa hadi kuwa mtu mzima. leo nitakuelezea hatua za ukuaji wa mtoto kisaikolojia muhimu sana katika malezi yake. hatua hizo ni kama ifatavyo 1.ORAL STAGE Mtoto anakua katika stage hii anapokuwa na umri wa,mwezi mmoja hadi mwaka mmoja.   Sasa kwa kipindi hiki erogenous zone ya mtoto inakua mdomoni, raha ya mtoto inakua kitu chochote kinachoingia mdomoni ndo maaana kipindi hiki mtoto kila kitu anachoshika anapeleka mdomoni . Hiki ndo kipindi cha kujenga strong bond kwa mtoto na mama pale mtoto anapokuwa ananyonya inamjenga kumthamini mama kuliko mtu yyte Kipindi hiki inabdi kuwa makini na vitu kama shanga,sarafu nk ambavyo akiweka mdomoni vnaweza kumkaba Hapa kama mzazi ana tabia ya kula kucha ndo kipindi mtoto nae anajifunza na kua hvo anapokua 2.ANAL STAGE Stage hii inaanza umri wa mwaka 1 hadi miaka mi 3 Hapa mtoto raha yake ni ...

KIDNEY FAILURE

TATIZO LA FIGO KUSHINDWA KUFANYA KAZI (RENAL/KIDNEY FAILURE) Dr. DALUS Figo ni miongoni mwa viungo muhimu sana katika mfumo wa utendaji kazi wa mwili wa binadamu. Kwa kawaida, mwili wa binadamu una figo mbili zenye maumbo yanayofanana kama yale ya maharage, yakiwa yamejificha nje ya utando unaozunguka tumbo, chini kidogo ya mbavu za chini.  Kazi za figo Kazi kuu za figo ni kuchuja vitu mbalimbali pamoja na sumu kadhaa katika damu na hivyo kusaidia katika kuhifadhi na kuthibiti kiwango cha maji na madini (electrolytes) mwilini. Katika kutekeleza hayo, figo huchuja vitu hivyo pamoja na maji yaliyo mwilini na kutengeneza mkojo, huchuja pia maji yasiyohitajika mwilini huku yakinyonya madini na kemikali muhimu kuzirudisha katika mzunguko wa damu na kutoa nje uchafu usiohitajika.  Kazi nyingine za mafigo ni ·         Kurekebisha na kuthibiti kiasi cha vitu mbalimbali katika damu pamoja na kiasi cha maji katika mwili · ...

UJAUZITO- MAZOEZI

KUFANYA MAZOEZI KIPINDI CHA UJAUZITO JE NI SALAMA? DOCTOR DALUS Kufanya mazoezi ni jambo ambalo binadamu wengi hulifanya mara kwa mara ikiwa ni mpango wa kimaisha au hulifanya mara moja moja. Mazoezi ni kitendo cha kuushughulisha mwili kwa njia mbalimbali. Mazoezi yaliyojipatia umaarufu ni kama kutembea, kukimbia, kushiriki michezo mbalimbali na hata watu hutumia vifaa maalumu vya mazoezi kuishughulisha miili yao. Hivi karibuni vituo vingi tuu vya mazoezi ambavyo vilikuwa maarufu kwenye nchi zilizoendelea vinaanza pia kuonekana barani Afrika. Mazoezi ni mazuri kwa afya ya mwili na akili. Na pia mazoezi yanahusishwa kabisa kisayansi kwenye jedwali la kupata afya bora. Ikiwa ni kawaida kabisa watu wa umri wowote ule kushiriki katika mazoezi, huwa inazua mjadala mara kwa mara ni kwa namna gani wajawazito wafanye mazoezi. Kwanza kabisa je wanaruhusiwa kisayansi kufanya mazoezi? Waandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya DW waliwahi kuyasema haya kuhusu mabadiliko ya mtazamo wa kisayansi kuh...